NIMR yatoa msaada wenye thamani zaidi sh.milioni Tano | Tarimo Blog

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), Profesa Yunus Mgaya akizungumza mara baada ya kukabidhi msaada katika Taasisi ya Ocean Road ikiwa ni maadhimisho ya miaka 40 ya NIMR ,jijini Dar es Salaam.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Ocean Road, Beatrice Erasto akizungumza katika kutoa shukrani Mara baada kukabidhiwa msaada kutoka Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) ,jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), Profesa Yunus Mgaya akimkabidhi sehemu ya msaada Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Ocean Road Beatrice Erasto ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 40 ya NIMR ,jijini Dar es Salaam.

Na Chalila Kibuda, Michuzi Tv

TAASISI ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) imetoa msaada vitu mbalimbali katika Taasisi ya Ocean Road vyenye thamani ya zaidi ya sh.milioni Tano (5).

Akizungumza mara baada ya kukabidhi msaada huo Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) Profesa Yunus Mgaya amesema kuwa katika kuadhimisha miaka 40 tangu kuanzishwa kwa Taasisi hiyo watoe msaada kwa kutambua Ocean Road ili kuweza kuwasaidia wagonjwa waliopo hapo.

Profesa Mgaya amesema kuwa licha ya kutoa msaada huo wataendelea kuwa karibu zaidi katika utoaji wa misaada mbalimbali.

"Tunaadhimisha Maadhimisho haya lakini tumetambua Ocean Road umhimu wa kuchangia nguvu zetu katika kuwasaidia wagonjwa kwani wanatoka sehemu mbalimbali ya nchi yetu na wakati mwingine wanaweza wakawa na changamoto ambazo sio za kimatibabu"amesema Profesa Mgaya 

Profesa Mgaya amesema katika Maadhimisho hayo wamefanya shughuli mbalimbali ikiwemo upimaji afya kwa wananchi bure kwa magonjwa ya kuambukiza na yale yasioambukiza.

Baadhi ya vitu walivyokabidhi ni sabuni za kuogea,Sabuni za Kufulia,Sabuni za Unga,Dawa za Meno,Maji,Maziwa ya Kopo ,Taulo,Kanga,Magauni aina ya Madela pamoja vifaa tiba.

Nae Kaimu Mtendaji wa Taasisi ya Ocean Beatrice Erasto amesema Kama Taasisi wanatoa shukrani kwa NIMR kutoa msaada kwao.

Amesema kuwa wanachangamoto lakini wadau wanapowaunga mkono katika kuwasaidia wanawatoa sehemu moja kwenda nyingine.


Mafunzo ya Ufugaji Bora na Matibabu, Jiunge sasa kwa KUBOFYA HAPA

0/Post a Comment/Comments

Previous Post Next Post

Ad

Ads1

Sponsor Ad

Ads2