KUTOKA HESLB-WADAIWA SUGU KUHUDUMIWA IJUMAA, JUMAMOSI NA JUMAPILI

Bodi ya mikopo ya Elimu ya juu Tanzania (HESLB) imetangaza kwanza, wadaiwa sugu wa mikopo watahudumiwa kwa siku za jumamosi na jumapili. Zikiwa zimebaki siku 11 kabla ya zoezi la kuwataka wadaiwa sugu kulipa madeni yao ndani ya siku 30, Ofisi za Bodi ya Mikopo zilizopo Mwenge, jijini Dar es Salaam zitakuwa wazi kwa siku mbili, Jumamosi, Disemba 3, 2016 na Jumapili, Disemba 4, 2016 kuanzia saa 3:00 asubuhi hadi saa 9:00 alasiri ili kutoa fursa muhimu kwa wadaiwa wote wa mikopo ya elimu ya juu ambao hawajaanza kurejesha mikopo yao kupata taarifa kuhusu madeni yao na kulipa.
 Njoo na Majina yako kamili, Chuo ulichosoma, Mwaka wa kuanza na wa kuhitimu, anuani yako ya
barua pepe (email), nambari ya simu yako ya kiganjani, mwajiri wako na Check Number yako iwapo umeajiriwa serikalini.
 Nyote mnakaribishwa ili kutumia fursa hii muhimu kabla ya zoezi kuhitimishwa na hatua za kisheria kuanza kuchukuliwa.
Kwa mawasiliano, waweza kuwasiliana na wahusika wa bodi ya mikopo kwa namba hizi hapa chini
Kwa mawasiliano zaidi piga 0763 459165 au 0767 513208.
 Tangazo hili limetolewa na:
MKURUGENZI MTENDAJI
BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU
02/12/2016.

0/Post a Comment/Comments

Previous Post Next Post

Ad

Ads1

Sponsor Ad

Ads2