Wajumbe wa Bunge la Kaunti ya Kirinyaga nchini Kenya, mwishoni mwa wiki walifanya ziara ya kutembelea kiwanda cha bia cha TBL cha Arusha ambapo walishuhudia shughuli za uzalishaji zinazoendeshwa na mifumo ya kisasa na teknolojia za hali ya juu .
Akiongea na ujumbe huo,Meneja wa kiwanda cha TBL cha Arusha,Joseph Mwaikasu, alieleza jinsi kampuni ya TBL Group mbali na kufanya uzalishaji kwa kutumia mifumo na teknolojia za kisasa katika viwanda vyake vilivyopo katika mikoa ya Mwanza,Arusha,Mbeya na Dar es Salaam inatekeleza sera ya ‘Dunia Maridhawa’ (Better world) ambayo imelenga kukuza viwanda sambamba na kuboresha shughuli za utunzaji wa mazingira , vyanzo vya maji na kuboresha maisha ya watu kwenye jamii ambapo kampuni imewekeza.
“Sera ya Dunia Maridhawa malengo yake yanashabihiana na Malengo Endelevu ya Milenia ya Umoja wa Mataifa (SDG’s) na sisi kama kampuni tunahakikisha tunafanikisha malengo haya na kwa kiasi kikubwa tumepata mafanikio hususani katika maeneo ya kufanya uzalishaji usio na athari kwa mazingira,matumizi mazuri ya maji ,kuendesha kampeni za utunzaji wa vyanzo vya maji,matumizi ya nishati mbadala zisizo na athari kwa mazingira,kuharibu taka kwa kutumia teknolojia za kisasa, na utakatishaji wa maji taka”.Alisisitiza Mwaikasu.
Wajumbe hao wakitembelea eneo la Kiwanda
Meneja wa kiwanda cha TBL cha Arusha,Joseph Mwaikasu,akiwaelezea mfumo wa uendeshaji kazi wa viwanda vya TBL Group
Picha mbalimbali zikionyesha wajumbe wakipata maelezo ya mchakato wa utengenezaji bia kutoka kwa wataalamu wa vitengo mbalimbali




SOMA ZAIDI




Post a Comment