SIMULIZI: WARIDI LA MAPENZI - SEHEMU YA MWISHO | Tarimo Blog.

WARIDI LA MAPENZI
SEHEMU YA TATU
Ilipoishia

Kwa mbali waliweza kumuona Suma akija huku amebeba mikoba yake. Alipofika kitu cha kwanza alimuuliza Mwalimu GG kama amemuona Sosi kwani alikuwa anamtafuta na hawezi kuondoka. Akaambiwa Sospeter ameshafika hapo na yuko ndani ya basi.
Endelea..........................

Penzi lao lilikua taratibu na miaka miwili baadaye walifunga pingu za maisha kabla tu ya kuanza masomo ya Chuo Kikuu. Waliishi pamoja Dar-es-Saalam wakati wote wa masomo hadi walipohitimu shahada zao za kwanza mwaka 1998. Wote waliajiriwa jijini hapo, Sospeter akifanya kazi katika idara ya Takwimu huku Suma akipata nafasi ya Ualimu katika shule ya sekondari ya Lugalo. Watu walionea wivu kwa jinsi walivyokuwa chanda na pete wakipendana kuliko kumbikumbi au njiwa. Waliheshimiana na kusaidiana katika kila hali. Ndio uchungu huu uliokuwa umekita kwenye moyo wa Suma akiwa bado amelala kitandani. Machozi yaliendelea kumbubujika.

“Suma, Suma, amka” Sauti ya upole ya kiume ilimshtua usingizini.
“Mume wangu Sosi” Suma aliendelea kulia huku akigalagala kitandani.
“Nini tena Suma, mbona unalia usingizini” Sauti hiyo iliendelea kuuliza huku mikono ya mtu huyo ikimtikisa, “umeota jinamizi mpenzi” Iliendelea sauti hiyo.
Suma hakuamini kusikia sauti hiyo, kwani haikuwa sauti ya mtu mwingine isipokuwa ya mume wake wa ndoa Sospeter Mkiru. Alifumbua macho yake taratibu kuangalia kama alikuwa bado anaota au ni kweli. Sospeter alikuwa ameketi kwenye ukingo wa kitandani huku akimuangalia mkewe kwa hofu na mahaba makubwa. Hajawahi kumuona akilia usingizini hata mara moja. Moyoni alijua ndoto yoyote aliyokuwa ameota hinti huyo ilikuwa ni mbaya kweli.
“Mpenzi, haya ni ndoto gani hiyo imekufanya ulie usingizini” alihoji huku kwa kutumia kidole gumba akimfuta machozi Suma.
“Jamani, hivi ni wewe kweli?” Suma aliinuka taratibu akaanza kuupapasa uso wa Sosi kuamini kama kweli ni yeye. Kwa mbali aliweza kusikia sauti za watoto zikicheza mchezo ya kombolela huku mlio wa magari ulisikika kwa mbali ukishindana na sauti za watoto hao. Alikuwa amelala na kanga moja tu kwani alijitupa kitandani baada ya kuoga akimsubiri mumewe atoke kazini.
“Ni mimi mpenzi” Sospeter alijibu kwa upole huku akimrushia busu. Alikumbuka mara ya kwanza kumbusu Suma miaka ile kule Karatu. Busu lake lilikuwa bado tamu na lenye mvuto usiochuja. Suma alimkumbatia mumewe na kumwomba Mungu amuepushe na mikosi yote, na maneno yote ya wamtakiao mabaya. Aliamua kumsimulia ndoto yake. Alipomaliza, alimuangalia mpenzi wake na kusubiri atasema nini.
“Mama Grace, tangu nikuone wewe kule Karatu sijaona mwanamke mwingine” Alisema kwa sauti ya kumhakikishia. “sijatamani wala sijaota kutamani mwanamke mwingine. Wote ninaowaona nikiwalinganisha na wewe, nitaendelea kukuchagua wewe hadi kaburini” Alisema huku macho yake yakilengwa na machozi. Suma alijikuta anatokwa na machozi tena, ingawa safari hii yalikuwa ni ya huba na furaha. Alimuuliza Mungu ilikuwaje astahili mwanamme namna hiyo.
Suma aliinuka kitandani, na kabla hajasimama vizuri kanga yake iliyokuwa bado imemning’inia mwilini ilidondoka, na kumwacha mtupu kama alivyozaliwa. Mwili wake wenye rangi ya maji ya kunde uliangaza kama mbalamwezi. Sosi alimuangalia mara moja na hamu yake ikamzidia. Alimvuta karibu huku yeye akiwa bado ameketi, alifungua miguu yake na kumsimamisha Suma katikati yake huku mikono yake ikiwa imezunguka makalio ya mviringo wa tufe. Alianza kumbusu tumboni , mapajani, huku vidole vyake vikiendelea kuyaminya minya makalio ya binti huo. Suma alinyanyua mguu wake wa kushoto na kuuweka juu ya ukingo wa kitanda. Harufu ya uanamke wake ilimwingia Sosi kama manukato ya thamani kutoka Yemeni. Kama fundi wa kukuna, Sosi alianza “kukuna nazi” na kukuna alikuna! Suma aliamua kujitupa kitandani, na kwa mahaba yasiyokifani walishirikiana tendo la ndoa bila hofu ya kubambwa au kufaminiwa. Hiyo ndiyo ilikuwa raha ya ndoa. Walipomaliza walijikuta wamelowa jasho utadhani walikuwa wanakimbia mchakamchaka.
“Haya niambie safari yako ya hospitali ilikuwaje” Sospeter alipata akili ya kuuliza kwani Suma alikuwa aonane na Daktari kwa uchunguzi wa kawaida.
“Una uhakika unataka kujua” Aliuliza kwa sauti ya upole iliyoficha jambo.
“Kido, nisingeuliza kama nisingetaka kujua” Alisema huku akimgeukia mkewe na kumtazama usoni. Suma aliuma mdomo wa chini kwa aibu za kike. Alimwangalia mumewe kwa mapenzi na kwa hamu.
“Unakumbuka wale mapacha uliokuwa unawazungumzia?” alimuuliza kwa haraka. Ulikuwa mtego ambao Sosi alinaswa kirahisi.
“Mapacha gani” aliuliza bila kujumlisha mbili na mbili.
“Kurwa na doto” Suma alijibu akicheka na kumuangalia usoni. Kama mtu aliyezibuliwa Sosi alifungua macho yake utadhani yako tayari kuchomoka kama ya Scooby Doo!
“Acha utani mama Grace!” Alisema
“Wala sikutanii, nimebeba mapacha!” Alisema kwa fahari kama mtu aliyetimiza wajibu wake. Sospeter alianza kucheka, kufurahi, na kushangilia utadhani amefunga goli lililoipeleka timu yake kwenye kombe la dunia Ujerumani! Alimvuta mke wake karibu na akiweka mkono wake kwenye tumbo la Suma, aliomba sala ya shukurani na baraka kwa viumbe hao wa Mungu. Mawazoni alianza kutafuta majina kama wote wakiwa wa kike, wa kiume au mchanganyiko. Suma alienda bafuni pembeni mwa chumba chao ambako alijisafisha na kubadili nguo. Alipotoka alikuwa anawaka. Alivalia gauni lake la rangi ya zambarau ya kifalme lenye madoa meupe, lilikokatwa kifuani kwa mtindo wa V na hivyo kuonesha kontua za matiti yake. Lilikuwa fupi lililombana kiunoni na kuishia magotini. Nywele zake zilizokuwa zimesukwa rasta zilidondoka mageni mwake utadhani binti ya mfalme. Alikuwa amejitia rangi nyekundu ya mdomo na wanja wa kope na nyusi. Alimalizia kwa kutinga viatu vyake vyenye ndefu kiasi huku vikiwa na kamba zilizozunguka miguu yake. Alikuwa na usafiri wa nguvu. Alisimama mbele ya kioo huku akijivisha hereni na mkufu uliokuwa na kito cha Tanzanite kifuani. Sospeter alijikuta akienda na kusimama nyuma yake, akimkumbatia toka nyuma, Suma alizungusha shingo yake na midomo yao ikagusana kwa busu lenye utamu wa pepo.
“Grace amesheenda kwa shangazi yake” Aliuliza Sosi
“Binamu zake walikuja kumchukua mara tu baada ya kutoka shule” Alijibu Suma. Jioni hiyo Sosi alimwambia wataenda kwenye ukumbi wa muziki ambako wana Sikinde walikuwa wanapiga. Suma alitangulia, na kufungua mlango wa mbele. Alipofungua nusura moyo wake ulipuke kwa mshtuko. Mbele yake kulikuwa na gari jeupe la kifahari la Limo, huku dereva wake akiwa ameshikilia mwamvuli mbele ya nyumba hiyo, akiwa naye amevalia suti nadhifu ya rangi nyeupe. Waswahili walikuwa wamekaa nje ya nyumba zao wakisubiri muda huo. Suma alimgeukia mpenzi wake na kupiga kelele ya furaha, machozi yakimtiririka tena. Waswahili walijikuta wakipiga makofi na vigelegele. Sospeter alimnong’oneza mpenzi wake, “Happy Valentine my love”! Suma aliishiwa nguvu. Waliingia ndani ya gari huku waswahili na watoto wa mtaani wakipiga minja na vigelegele. Moyoni, Suma aliapa atamrudishia fadhila mumewe usiku huo.
Mwisho


0/Post a Comment/Comments

Previous Post Next Post

Ad

Ads1

Sponsor Ad

Ads2