BASHUNGWA AWAPONGEZA MUHIMBILI KWA KUTENGENEZA VAZI MAALUMU LA WAUGUZI. | Tarimo Blog

Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Innocent Bashungwa ameupongeza uongozi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa kutengeneza mavazi maalum (coverall) za wauguzi ambayo yanasaidia wahudumu wa afya kujikinga na ugonjwa wa Corona.

“Nawapongeza hospitali ya Taifa Muhimbili kwa kutengeneza mavazi maalum (coverall) ya wauguzi Mungu awabariki na kuwalinda wauguzi wetu”.

Aidha, amevipongeza viwanda vyote nchini kwa kuendelea kuhakikisha vinatoa mchango mkubwa kwa kipindi hiki cha kupambana na ugojwa wa Corona na ametoa wito kwa viwanda na mtanzania yeyote anaeweza kutengeneza mavazi maalum ya wauguzi ajitokeze na awasiliane na Wizara ya Viwanda na Biashara.

“Viwanda vyetu nchini hamjawahi kuniangusha, yeyote anayeweza kutengeneza awasiliane na Wizara ya Viwanda na Biashara namba ya simu +255784218155" ili kupata muongozo.






Mafunzo ya Ufugaji Bora na Matibabu, Jiunge sasa kwa KUBOFYA HAPA

0/Post a Comment/Comments

Previous Post Next Post

Ad

Ads1

Sponsor Ad

Ads2