MTOTO WA MIAKA TISA AOMBA MSAADA KWA WASAMARIA WEMA AKAPATE MATIBABU YA MOYO MUHIMBILI | Tarimo Blog


NA  YEREMIAS  NGERANGERA…NAMTUMBO
Mtoto mwenye umri wa miaka  tisa na mwanafunzi wa darasa la tatu  katika shule ya msingi Likuyuseka wilayani Namtumbo  mkoani Ruvuma Jeska James Kifaru anaomba kutoka kwa wasamaria wema kumsaidia mchango wa fedha ili aweze  kwenda matibabu ya moyo katika hospitali ya Taifa Muhimbili  baada ya wazazi wake kutokuwa na uwezo wa kumfikisha katika hospitali hiyo.
Akiongea akiwa katika ofisi ya Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo  Jeska alisema anaomba msaada kwa wasamaria waweze kumchangia fedha ili aweze  kwenda kutibiwa moyo katika  hospitali ya  taifa muhimbili baada ya wazazi wake kushindwa kumpeleka huko kutokana na kipato duni.
Mama  mzazi wa Jeska  aitwaye Stamili Abdallah Gehu alisema  walifika ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Namtumbo kuomba kibali  cha mkuu wa wilaya  cha kuomba kuchangisha mchango fedha na wakafanikiwa kupata kibali hicho na sasa wanapita mitaani kuchangisha fedha hizo ili waweze kumpeleka kijana wao hospitali.
Stamili alisema  walimpeleka kijana wao matibabu katika kituo cha afya Namtumbo mwezi januari  mwaka huu na kasha kushauriwa na daktari wampeleke hospitali ya peramiho na walipofika katika hospitali ya peramiho aligundulika na tatizo la moyo hivyo akapewa dawa za kutumia mwezi mzima  na alipomaliza alirejea katika hospitali hiyo tarehe 28 mwezi huo januari na kushauriwa kumpeleka kijana wao huyo hospitali ya Taifa muhimbili. 
Hata hivyo wanaendelea kutumia dawa kutoka katika hospitali ya peramiho huku wakimwona kijana wao huyo akibadili rangi  na kuwa Mweusi badala ya rangi yake ile ya awali kuanza kutoweka kila kukicha .
Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Likuyuseka  Bonifasi  Sichela alisema mwanafunzi wake  Jeska  anahudhuria shule na kuipenda shule licha ya kuwa mdhaifu na kutoonesha furaha mara kwa mara darasani  kwa kusumbuliwa na moyo lakini  anafanya vyema masomo yake. 
Wazazi wa Jeska ,James Flavian kifaru  naStamili  Abdaallah  Gehu wanaishi katika kijiji cha Likuyuseka ambao kipato chao ni duni  wanawaomba wasamaria wema msaada wa fedha kupitia namba zao za simu ya mkononi 0715490997  simu waweze kumpeleka mtoto wao hospitali taifa  muhimbili.


Mafunzo ya Ufugaji Bora na Matibabu, Jiunge sasa kwa KUBOFYA HAPA

0/Post a Comment/Comments

Previous Post Next Post

Ad

Ads1

Sponsor Ad

Ads2