KITABU CHA MBIO ZA MWENGE CHAZINDULIWA | Tarimo Blog

.Viongozi mbalimbali wakiwa katika picha ya pamoja wakionyesha kitabu maalum chenye ratiba ya Mbio za Mwenge wa Uhuru 2021 ambazo zitazinduliwa Mkoa wa kusini Unguja Mwehe  tarehe 17 Mei 2021 na kilele cha mbio hizo kufanyika mkoani Geita tarehe 14 oktoba 2021,kauli mbiu kwa mwaka huu ni “Tehama ni msingi wa Taifa Endelevu ,itumie kwa usahihi na Uwajibikaji”

Kaimu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Lela Muhamed Mussa akisoma taarifa maalum kwa vyombo vya habari juu ya suala zima la Uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru unaotarajiwa kufanyika katika Uwanja wa Mwehe Makunduchui Mkoa wa Kusini Unguja tarehe 17 Mei 2021 ambapo kauli mbiu ni “Tehama ni msingi wa Taifa Endelevu, itumie kwa usahihi na Uwajibikaji” hafla iliyofanyika Ukumbi wa Wizara ya Utalii na Mambo ya kale Kikwajuni Zanzibar.

Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anaeshughulikia Maswala ya Ulemavu Vijana, Sera na Uratibu wa Shughuli za Bunge Jenista Mhagama akitoa historia ya mwenge wa uhuru na kutolea ufafanuzi faida zinazopatikana katika mbio za Mwenge huko Ukumbi wa Wizara ya Utalii na Mambo ya kale Kikwajuni Zanzibar.
Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anaeshughulikia Maswala ya Ulemavu, Vijana, Sera na Uratibu wa Shughuli za Bunge Jenista Mhagama (kulia) akimkabidhi Kaimu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Lela Muhamed Mussa vitabu maalum vya mbio za Mwenge wa uhuru 2021 aweze kukata utepe ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa vitabu hivyo vitakavyomfikia kila mtu kupitia Ofisi za Wilaya hafla iliyofanyika Ukumbi wa Wizara ya Utalii na Mambo ya kale Kikwajuni Zanzibar.

 
 


Mafunzo ya Ufugaji Bora na Matibabu, Jiunge sasa kwa KUBOFYA HAPA

0/Post a Comment/Comments

Previous Post Next Post

Ad

Ads1

Sponsor Ad

Ads2