Moto wateketeza bweni shule ye sekondari Ikuwo wilayani Makete | Tarimo Blog




Na Amiri Kilagalila,Njombe
BWENI la wasichana shule ya Sekondari Ikuwo wilayani Makete mkoani Njombe limeteketea kwa Moto huku ikisadikika chanzo chake kuwa ni hitilafu ya Umeme au mkaa ulioanzia Chumba cha Matron (Mlezi wa wanafunzi)

Moto huo ulioanza asubuhi leo majira ya saa moja umeteketeza vitanda vitanda, magodoro, nguo za wanafunzi pamoja na vifaa vyao huku wanafunzi wote wakiwa salama

Jumla ya thamani ya vitu vilivyoteketea bado haijajulikana huku tathmini ikiendelea kufanyika.

Kamati ya ulinzi na usalama Wilaya, Mkurugenzi mtendaji wilaya na wataalamu mbalimbali wamefika kuangalia mali zilizoteketea kwa Moto huo uliotokea
Chanzo:Kitulo FM

Mafunzo ya Ufugaji Bora na Matibabu, Jiunge sasa kwa KUBOFYA HAPA

0/Post a Comment/Comments

Previous Post Next Post

Ad

Ads1

Sponsor Ad

Ads2