MWENGE WA UHURU WATEMBELEA KITUO CHA KUSUKUMIA MAJI CHA MAKONGO | Tarimo Blog

 

Mkurugenzi wa Miundombinu na Uwekezaji DAWASA Mhandisi Ramadhani Mketo akitoa ufafanuzi kwa Kiongozi wa Mbio Maalumu za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2021, Luteni Josephine Mwambashi na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Godwin Gondwe kuhusu mradi wa kituo cha kusukuma maji  uliopo katika Kata la Makongo Juu katika Manispaa ya Kinondoni mkoani wa Dar es Salaam  unavyotoa huduma wakati wa ziara ya Mwenge ulipotembelea mradi huo uliotekelezwa na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)
Mkuu wa kitengo cha ubora na viwango kutoka DAWASA Injinia Christopher Christian akitoa taarifa kuhusu ujenzi wa mradi wa kituo cha kusukuma maji  pamoja na usambazaji wa maji katika maeneo mbalimbali ya mkoa wa Dar es Salaam uliopo katika Kata la Makongo Juu katika Manispaa ya Kinondoni mkoani humo mara baada ya Mwenge wa Uhuru kutembea mradi huo leo
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Godwin Gondwe akizungumza wakati wa Ziara ya Mwenge wa Uhuru katika mradi wa kituo cha kusukuma maji uliopo Kata la Makongo Juu katika Manispaa ya Kinondoni mkoani wa Dar es Salaam  mara baada ya kumalizika kwa Ukaguzi wa mradi huo leo wakati wa Mbio za Mwenge zilizotembelea kituo hicho.
Kiongozi wa Mbio Maalumu za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2021, Luteni Josephine Mwambashi akizungumza mara baada ya kutembelea na kukagua mradi wa kituo cha kusukuma maji uliopo Kata la Makongo Juu katika Manispaa ya Kinondoni mkoani wa Dar es Salaam wakati wa Ziara ya Ukaguzi wa mradi huo zilizofanywa na Mwenge wa Uhuru leo.
Mkurugenzi wa Miundombinu na Uwekezaji DAWASA Mhandisi Ramadhani Mketo akitoa ufafanuzi akitoa ufafanuzi kwa Kiongozi wa Mbio Maalumu za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2021, Luteni Josephine Mwambashi pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Godwin Gondwe kuhusu kituo hicho kinavyofanya kazi hasa pampu zinazotumika kusukumia maji na kusambaza maeneo mbalimbali ya mkoa wa Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Miundombinu na Uwekezaji DAWASA Mhandisi Ramadhani Mketo akitoa maelezo kwa Kiongozi wa Mbio Maalumu za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2021, Luteni Josephine Mwambashi alipokuwa anakagua akishirikiana na wenzake.
Mwenge wa Uhuru ukiingia katika mradi wa kituo cha kusukumia maji kilichopo Kata ya Makongo ukiongozwa na Kiongozi wa Mbio Maalumu za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2021, Luteni Josephine Mwambashi pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Godwin Gondwe.

Baadhi ya mitambo za kusukumia maji iliyopo kwenye mradi wa Makongo Juu


Mafunzo ya Ufugaji Bora na Matibabu, Jiunge sasa kwa KUBOFYA HAPA

0/Post a Comment/Comments

Previous Post Next Post

Ad

Ads1

Sponsor Ad

Ads2