TIA, GOLDEN NATION YAWANOA WANAFUNZI VYUO VIKUU | Tarimo Blog

 

Mkurugenzi wa kampuni ya Golden Nation Lameck John akizungumza na wanafunzi waliojitokeza katika jukwaa maalumu la ''Mind Set Event'' na kuwashauri wanafunzi hao kutokata tamaa katika safari ya kutimiza malengo yao, Leo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Kaampuni ya Jeannele Corporate Solution Jeremia Kahurananga akitoa mada katika warsha hiyo ambapo amewataka wanafunzi kushirikiana na kutoacha kutafuta fursa zitakazowajenga kifikra na mawazo, leo jijini Dar es Salaam,
Mmoja wa wakufunzi wa Taasisi ya Uhasibu Nchini (TIA,) akitoa mada katika warsha hiyo ambapo amewataka wanafunzi kujenga na kuimarisha uwezo wa kufikiri kwa kusoma vitabu, kufanya mazoezi na kula vyakula vyenye tija kwa afya, leo jijini Dar es Salaam.


Majadiliano yakiendelea.


TAASISI ya uhasibu Nchini (TIA,)kwa kushirikiana na kampuni ya Golden Nation wametoa mafunzo maalumu kupitia jukwaa  la ''Mind set event'' kwa wanafunzi wa vyuo vikuu nchini yakilenga kuwajengea uwezo kufanya maamuzi  na fikra zaidi katika kujiandaa na safari pindi wamalizapo masomo yao na kurejea katika jamii.

Akizungumza katika mafunzo hayo Mkurugenzi wa Kampuni ya Golden Nation Lameck John amesema kuwa, lazima vijana wafikiri zaidi ni nini watafanya kwa jamii yao kwa baadaye na kuwataka vijana hao kuwa na malengo  na kuzitumia fursa zaidi na sio kufikiri katika kuajiriwa pekee.

''Kwa hatua tuliyofikia hapa lazima tuoneshe ukomavu wa fikra kwa kuchakata maarifa tuliyopewa darasani kwa kuyahusianisha na fursa zilizopo katika jamii, na hiyo ni kwa kushirikiana na walimu pamoja na sisi vijana kwa kuhakikisha kuwa tunashikana mikono na kila mmoja wetu anatimiza ndoto zake.'' Amesema.

Aidha amewashauri wanavyuo hao kutumia fursa zitokanazo na mitandao ya kijamii kutimiza malengo yao na hiyo ni pamoja na kusoma pamoja na kutangaza masuala yenye tija kwao na jamii kwa ujumla.

Vilevile  ameeleza kuwa, ushirikiano  ya wahitimu una nguvu katika kuhakikisha maendeleo na mafanikio yanafikiwa kwa kila mmoja bila kutegemea ajira za moja kwa moja.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Jeannelle Corporate Solution Jeremia Kahurananga amewashauri wanavyuo hao kuweka mbele na kuendelea kupata elimu ya utambuzi ili waweze kufanya mambo makubwa zaidi wanayowaza kuyafanya.

''Elimu haina mwisho, na kwa hatua hii mliyofikia ni vyema mkawa mnahudhuria warsha za aina hii ambazo kwa kiasi kikubwa zinawaandaa na namna ya kukabiriana na changamoto za ajira.....ukipata somo katika warsha hizi unaweza kujiandaa vizuri kifikra kwa kutotegemea ajira za moja kwa moja bali kujiajiri wewe mwenyewe,'' Amesema.

Kahurananga amekishukuru Chuo cha TIA kwa kuendelea kutoa mafunzo ya namna hiyo kwa wanafunzi wao na kusema kuwa  hafla hiyo iliyoandaliwa na Chuo hicho kwa kushirikiana na Golden Nation itumike kama chachu kwao na vyuo vingine kwa kuwafanya vijana kufikiri  zaidi ni nini watafanya kwa manufaa yao jamii na vijana katika jamii.


Mafunzo ya Ufugaji Bora na Matibabu, Jiunge sasa kwa KUBOFYA HAPA

0/Post a Comment/Comments

Previous Post Next Post

Ad

Ads1

Sponsor Ad

Ads2