ZIARA YA MHESHIMIWA WAZIRI MKUU MKOANI MBEYA | Tarimo Blog



Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizindua Chuo cha Ufundi Stadi cha wilaya ya Busokelo mkoani Mbeya, Agosti 1, 2021. Wengine pichani kutoka kushoto ni Naibu Spika wa Bunge, Dkt. Tulia Ackson, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Juma Homera, Waziri wa Elimu, Sayansi na Tekinolojia, Profesa Joyce Ndalichako na kulia ni Mbunge wa Busokelo, Atupele Mwakibete. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na aliyekuwa Waziri katika serikali ya Awamu ya Nne, Profesa Mark Mwandosya (kulia) na mkewe Lucy Mwandosya (wa pili kulia) wakati alipowasili kwenye viwanja vya Chuo cha Ufundi cha wilaya ya Busokelo mkoani Mbeya kuzindua Chuo hicho, Agosti 1, 2021. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa leo Agosti 1, 2021 amekabidhiwa zawadi ya picha aliyopiga akivuka mto Rufiji kwa kutumia ngalawa mwaka 2010 akiwa Mkuu wa wilaya ya Rufiji wakati alipompokea Profesa Mark Mwandosya aliyekuwa ni Waziri katika serikali ya Awamu ya Nne. Picha hiyo ilikabidhiwa kwake na Profesa Mwandosya (kushoto) na mkewe Lucy Mwandosya (wa pili kushoto) baada ya Mheshimiwa Majaliwa kuzindua Chuo cha Ufundi Stadi cha wilaya ya Busokelo mkoani Mbeya. Wa pili kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Juma Homera. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)


Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitazma kaunda suti wakati alipotembelea darasa la mafunzo ya ushonaji nguo katika Chuo cha Ufundi Stadi cha wilaya ya Busokelo mkoani Mbeya, Agosti 1, 2021. Kushoto ni Waziri wa Elimu, Sayansi na Tekinolojia, Profesa Joyce Ndalichako. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) 


Mafunzo ya Ufugaji Bora na Matibabu, Jiunge sasa kwa KUBOFYA HAPA

0/Post a Comment/Comments

Previous Post Next Post

Ad

Ads1

Sponsor Ad

Ads2