BAADA YA KUWA NAMBA MOJA KATIKA UUZAJI MAFUTA PUMA ENERGY TANZANIA SASA KUANZA KUUZA GESI ZA MAJUMBANI | Tarimo Blog

KAMPUNI namba moja katika uuzaji wa mafuta nchini Tanzania ya Puma Energy imetoa tuzo kwa Mawakala wake wa kuuza mafuta huku ikitumia nafasi hiyo kutoa muelekeo wake katika kujiimarisha zaidi kibiashara.

Akizungumza wakati wa utoaji huo wa tuzo,Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Kampuni ya Mafuta ya Puma Tanzania Dk.Seleman Majige amesema baada ya kufanikiwa katika uuzaji mafuta sasa wanataka kuanzia Mei mwaka huu kuuza gesi za majumbani.Gesi hiyo itauzwa kwenye vituo vya mafuta vya Kampuni hiyo kote nchini.

Dkt.Majige amesema kuwa kwakuwa kampuni ya Mafuta ya Puma Energy ndio namba moja na yenye huduma bora hapa nchini hivyo hata kwenye uuzaji na usambazaji wa nishati hiyo ya gesi watakuwa namba moja kama ilivyo kawaida yao.

"Nitumie nafasi hii kuwapongeza Mawakala wote waliopata tuzo hizi na kwakweli tunajivunia kwa huduma bora ambazo mnazifanya na niwaombe mkaendelee kuitangaza, na kuilinda Puma Energy limited ili iendelee kuwa kampuni namba moja kwa ubora.

"Na hivi karibuni tunakwenda kuaza kufanya huduma ya biashara ya usambazaji gesi ya majumbani ,tayari bodi imeshakaa na kupitisha hilo,hivyo matarajio yangu nikuona tunaendelea kuwa namba moja kwa ubora wa huduma zetu hivyo nawapongeza nyote kwa kazi nzuri mnayofanya. "amesisitiza Dk.Majige.

Kuhusu Kampuni hiyo amesema kuwa wameendelea kuwa namba moja kwani kila kituo cha Puma ambacho utakwenda utakuta huduma hiyo ya mafuta na hivi sasa wameongeza vituo kutoka 52 vya awali na kufikia vituo 80 lakini lengo ni kuona hadi kufikia mwaka 2025 wanakuwa na vituo 150 na sio 100.Hivyo ametoa rai kwa Menejimenti ya Kampuni hii ya Puma hadi kufikia mwaka 2025 wawe wameongeza vituo hadi kufikia 150 na sio 100 kama walivyokuwa wamepanga.

Dk.Majige amewakumbusha wadau hao kuwa Puma ni kampuni kubwa hivyo waendelee kuilinda na kuhakikisha mafuta yanakuwa salama huku akiiitaka menejimenti kuweka mkakati wa kuaziasha vituo vijijini ili kuhakikisha huduma hiyo inawafikia wananchi wengi zaidi.

Amesisitiza umuhimu wa lugha na matendo mazuri ya mawakala wakati wanawahudumia wateja wa Kampuni hiyo kwani hiyo ndio silaha ya Puma Energy Tanzania kuendelea kuwa namba moja.

Kwa upande wake Miurugenzi Mtendaji wa Puma Tanzania Dominic Dhanah amesema Kampuni hiyo ndio inayoongoza nchini na inashika namba moja kwa ubora.

Amesema kuwa namba moja ni kazi kubwa sana lakini wataendelea kuwekeza nakwamba hadi kufikia sasa Puma inavituo 80 kutoka vituo 52 vilivyokuwepo hapo mwanzo na lengo nikufikisha vituo 100 kufikia mwaka 2025.

"Ndugu Mgeni rasmi kampuni imeendelea kuwa wabunifu na tumeongeza huduma nyingine ya vilainishi vya kwenye magari na mapema mwaka huu tunatarajia kuzindua nishati ya gesi ya majumbani ambayo itakuwa inapatikana kwenye vituo vyetu vyote na hakuna shaka kwamba itapokelewa vizuri. "Amesema Dhanah

Aidha amewapongeza watoa huduma wote wa Puma kwani wao ndio wamekuwa chachu ya mafanikio ya kampuni hiyo huku akiwataka waendelee kufanya vizuri zaidi na katika tuzo hizo kituo cha mafuta kutoka Arusha Cetral Station kimefanikiwa kuwa mshindi wa jumla wa uuzaji wa mafuta kwa mwaka wa pili mfululizo.


Ilikuwa ni shangwe furaha nderemo na vifijo kwa waliojishindia zawadi mbalimbali siku hiyo




Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Puma Energy Tanzania Dkt. Selemani Majige akimkabidhi zawadi mshindi wa mawakala wa jumla wa vituo vya mafuta waliofanya vizuri katika vituo vya kampuni hiyo iliyofanyika hibi karibuni lJijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Puma Energy Tanzania Dkt. Selemani Majige akizungumza kwenye hafla ya utoaji wa Zawadi kwa mawakala (Dealers) wa vituo vya mafuta vya Puma Energy nchini iliyofanyika hivi karibuni Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Puma Energy Tanzania Bw. Dominic Dhanah akizungumza kwenye hafla ya utoaji wa Zawadi kwa mawakala (Dealers) wa vituo vya mafuta vya Puma Energy nchini iliyofanyika hivi karibuni Jijini Dar es Salaam.

Wageni waalikwa mbalimbali wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri ukumbini humo
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Puma Energy Tanzania Dkt. Selemani Majige akifurahia jambo na Mkurugenzi Mtendaji wa Puma Energy Tanzania Bw. Dominic Dhanah kwenye hafla ya utoaji wa Zawadi kwa mawakala (Dealers) wa vituo vya mafuta vya Puma Energy nchini iliyofanyika hivi Karibuni Jijini Dar es Salaam



Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Puma Energy Tanzania Dkt. Selemani Majige akimkabidhi zawadi mawakala mbalimbali waliofanya vizuri kwenye vituo vya mafuta vya kampuni ya Puma Energy Tanzania katika hafla ya utoaji wa Zawadi kwa mawakala (Dealers) wa vituo vya mafuta vya kampuni hiyo nchini iliyofanyika hivi karibuni Jijini Dar es Salaam.








Mafunzo ya Ufugaji Bora na Matibabu, Jiunge sasa kwa KUBOFYA HAPA

0/Post a Comment/Comments

Previous Post Next Post

Ad

Ads1

Sponsor Ad

Ads2