MBUNGE WA BABATI VIJIJNI ATOA MABATI 600 KUKAMILISHA MIRADI YA ELIMU NA AFYA | Tarimo Blog






Na John Walter-Babati

Mbunge wa Jimbo la Babati Vijijini Daniel Sillo ametoa mabati 600 kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa miradi ya elimu na afya jimboni humo.

Hafla ya makabidhiano hayo imefanyika leo agosti 26,2022 katika ofisi za Halmashauri ya wilaya ya Babati ikiwa ni mkakati wa Mbunge huyo (CCM) kusaidia kukamilisha miradi ya afya na elimu inayoendelea kujengwa wilayani hapo.

Mbunge huyo ametoa mabati hayo kwa mgawanyo katika vijiji sita vya Tsamas (150), ,Secheda (117),Boay (84),Kisangaji (29),Datar (110) na Yorotonik (110).

Amewataka madiwani na watendaji wengine kusimamia bati hizo zikatumike kwenye miradi iliyokusudiwa.

Aidha ameishukuru benki ya NMB kwa msaada huo walioutoa ambao umetokana na mahusiano mazuri waliyonayo yeye na benki hiyo.

Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Babati imempongeza Mbunge Sillo kwa jitihada za kuwaletea wananchi maendeleo kama inavyoelekeza ilani ya chama cha Mapinduzi (CCM).

Akizungumza kwa niaba ya madiwani, diwani wa kata ya Ufana Bernad Bajuta amesema mabati hayo yatasaidia sana kumaliza miradi ya elimu na afya iliyokwama kwa muda mrefu.


Mafunzo ya Ufugaji Bora na Matibabu, Jiunge sasa kwa KUBOFYA HAPA

0/Post a Comment/Comments

Previous Post Next Post

Ad

Ads1

Sponsor Ad

Ads2