MWINYI AZINDUA MKUTANO MKUU WA AMANI ZANZIBAR | Tarimo Blog

 




RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amesema kuwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa imeundwa kwa lengo la kuendeleza na kudumisha amani, umoja na mshikamano miongoni mwa wananchi wa Zanzibar.

Dk. Hussein Mwinyi aliyasema hayo leo katika hotuba yake ya ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Pili wa Amani uliofanyika huko katika ukumbi wa Hoteli ya Zanzibar Beach Resort, Mazizini nje kidogo mwa Jiji la Zanzibar.

Katika maelezo yake Rais Dk. Mwinyi alisema kuwa  Mkutano huo umefanyika wakati muafaka ambapo nchi imefanikiwa kufanya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020 katika hali ya amani na ulivu mkubwa.

Amesema kwamba suala la kuendeleza na kudumisha amani hapa Zanzibar limepewa kipaumbele katika Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 pamoja na mipango ya maendeleo ya Kitaifa.

Rais Dk. Mwinyi aliongeza kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ya Awamu ya Nane itaendelea kufanya kila linalowezekana kwa ajili ya kuendeleza fikra za waasisi wa nchi hii na viongozi waliotangulia katika kudumisha umoja na mshikamano wa wananchi wa Zanzibar.

Aliongeza kuwa ni ukweli usio na shaka kwamba maendeleo hayawezi kupatikana katika nchi yoyote bila ya kuwepo amani na mshikamano.

Kwa msingi huo, Dk. Mwinyi aliwahimiza viongozi wa vyama na Serikali, viongozi wa dini na madhehebu mbali mbali, vyombo vya habari, wazee na vijana katika jamii.


Mafunzo ya Ufugaji Bora na Matibabu, Jiunge sasa kwa KUBOFYA HAPA

0/Post a Comment/Comments

Previous Post Next Post

Ad

Ads1

Sponsor Ad

Ads2