

Programu hii imezinduliwa kipindi muafaka ambacho Serikali na wadau wa maendeleo nchini wanawekeza nguvu kubwa katika kuhakikisha wahitimu wa vyuo vikuu nchini wanapata ajira na kutengenezewa mazingira ya kujiajiri.

“Mpaka sasa ni miezi mitano tokea vijana hawa wajiunge katika program hii. Kama Benki tunajivunia kuwa sehemu ya suluhisho la ajira kwa vijana,” alisema Kishimbo huku akibainisha kuwa baada ya miaka mitatu ya kuhitimu vijana wengine wanaohitimu vyuo vikuu wataajiriwa kupitia programu hiyo.

Akitoa salamu za shukrani kwa niaba ya washiriki wa program hiyo, Aurelia Haule aliushukuru uongozi wa Benki ya CRDB kwa kutoa fursa ya mafunzo na ajira kwa vijana. Alisema kwa kipindi cha miezi mitano ya walichojiunga na benki hiyo wamejifunza vitu vingi kuhusiana na uendeshaji na usimamizi wa benki. “Ni imani yangu kuwa baada ya programu hii tutakwenda kuwa wabobevu na kuisaidia benki yetu kupiga hatua kubwa kiutendaji,” aliongezea Aurelia.
Mafunzo ya Ufugaji Bora na Matibabu, Jiunge sasa kwa KUBOFYA HAPA
Post a Comment